Kisha akapanga kuni vizuri, akakata vipandevipande ile ngombe dume, akaviweka juu ya kuni. Kisha akawaambia watu: “Mujaze mitungi mine maji muimwangie juu ya sadaka hii ya kuteketezwa pamoja na kuni.” Wakafanya hivyo.
Basi, Ahabu akaenda zake kula na kunywa. Naye Elia akapanda juu ya kilele cha mulima Karmeli, na kule akainama uso mpaka chini na kuuweka uso wake katikati ya magoti yake.
Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.
Yesu aliposikia habari hii, akaondoka pale ndani ya chombo, na kwenda peke yake kwa pahali penye ukiwa. Nayo makundi ya watu waliposikia vile, wakatoka katika miji yao na kumufuata Yesu kwa miguu.
Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.
Hii ni safari yangu ya tatu ninayotayarisha kuja kwenu. Kama Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kila neno linapaswa kuhakikishwa kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu.”
Yeye atabadilisha huu mwili wetu wa uzaifu na kuufananisha na mwili wake wa utukufu kwa nguvu ambayo kwa njia yake anaweza kuwa na mamlaka juu ya vitu vyote.