Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Marko 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Huyu si yule museremala, mwana wa Maria, ndugu ya Yakobo, Yose, Yuda na Simoni? Nao wadada zake, si wanaishi hapa kati yetu?” Na kwa hiyo wakakosa kumwaminia.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Marko 6:3
21 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Heri mutu yule mimi sitakayekuwa kikwazo kwake!”


Yesu alipokuwa hajamaliza kusema na lile kundi la watu, mama yake na wandugu zake wakafika. Walisimama inje wakitaka kusemezana naye.


Kulikuwa wanawake wamoja walioangalia kwa mbali. Kati yao kulikuwa Maria wa Magdala, Maria mama ya kijana Yakobo na Yose na mwanamuke mwingine Salome.


Andrea na Filipo, Bartolomayo, Matayo, Toma, Yakobo mwana wa Alfayo, Tadeo, Simoni wa kundi la Wazeloti


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


Heri mutu yule ambaye sitakuwa kikwazo kwake.”


Halafu watu wakamwambia Yesu: “Mama yako na wandugu zako wanasimama inje, wanataka kukuona.”


Yuda (si yule Yuda Iskariota) akamwuliza: “Bwana, namna gani utajitambulisha mwenyewe kwetu wala si kwa dunia?”


Nao wakasema: “Huyu si Yesu mwana wa Yosefu? Si tunawajua baba yake na mama yake? Namna gani anaweza kusema sasa kwamba alishuka toka mbinguni?”


Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


Naye akawanyamazisha kwa kunyoosha mukono, kuwaelezea namna Bwana alivyomwondoa katika kifungo. Akawaambia tena: “Muwaelezee Yakobo na wandugu wengine waamini habari hizi.” Kisha Petro akaondoka na kwenda nafasi ingine.


Lakini sisi tunamuhubiri Kristo aliyetundikwa juu ya musalaba, na mahubiri hayo yanahesabiwa kama kikwazo kwa Wayuda na upumbafu kwa watu wa mataifa mengine.


basi sina haki ya kupokea chakula na kinywaji kwa ajili ya kazi yangu?


Sikumwona mutu mwingine isipokuwa tu Yakobo, ndugu ya Bwana.


Mumwendee Bwana. Yeye ni jiwe lenye uzima. Jiwe lile lilitupiliwa na watu lakini lilichaguliwa na Mungu, nalo linahesabiwa kuwa la bei kali mbele yake.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yuda, mutumishi wa Yesu Kristo na ndugu wa Yakobo. Ninawaandikia ninyi mulioitwa na Mungu Baba na munaoishi katika upendo wake na kulindwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις