Nafasi ile mbegu zilipoanguka pembeni ya njia, ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu, lakini mara moja Shetani anakuja na kuondoa lile Neno lililopandwa ndani yao.
Lakini halizami ndani yao kama mizizi; wanalishika kwa muda mufupi tu. Wakati taabu na mateso vinapowafikia kwa ajili ya Neno la Mungu, mara moja wanaanguka.
Herode alimwogopa Yoane, kwa sababu alijua kwamba Yoane ni mwenye haki na mutakatifu. Kwa hivi alimulinda. Alipenda kumusikiliza, ijapokuwa alifazaika sana kila mara alipomusikia.
Udongo wenye mawe pahali mbegu zilipoanguka ni mufano wa watu wanaosikia neno na kulipokea kwa furaha, lakini halizami ndani yao kama mizizi. Wanaliaminia kwa muda mufupi tu, nayo majaribu yanapowafikia, wanaliacha.
Hata Simoni vilevile akaamini na kubatizwa. Na nyuma ya pale alishikamana na Filipo, naye alishangaa sana alipoona kitambulisho kikubwa na miujiza iliyokuwa ikifanyika.