41 Wanafunzi wengine kumi waliposikia maneno yale, wakachukizwa na Yakobo na Yoane.
Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.
Mupendane ninyi kwa ninyi kwa kweli kama vile wandugu, nanyi muheshimiane ninyi kwa ninyi.
Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.
Musizani kwamba ni kwa bure Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anasikia wivu sana kwa ajili ya yule Roho aliyemuweka akae ndani yetu.”
Kulitokea ubishi kati ya wanafunzi wa kujua nani anayekuwa mukubwa kati yao.
Wanafunzi wengine kumi waliposikia maneno yale, wakachukizwa na wale wandugu wawili.
Yesu akawaita wote na kuwaambia: “Munajua kwamba wale wanaohesabiwa kuwa watawala wa mataifa wanayatawala kwa kinguvu, na wakubwa yao wanayagandamiza.
Yesu akawaambia: “Wafalme wa mataifa wanawatawala watu wao kwa nguvu; na wale wenye mamlaka juu yao wanajiita ‘Watenda mema.’