26 Wanafunzi waliposikia maneno hayo wakazidi kushangaa hata wakaulizana wao kwa wao: “Ni nani basi anayeweza kuokolewa?”
Nao wakajibu: “Umwamini Bwana Yesu, nawe utaokolewa pamoja na watu wote wa nyumba yako.”
Sasa nitasema kama mwenda-wazimu: wao ni watumishi wa Kristo? Mimi ni mutumishi wake zaidi kuliko wao. Nimetumika kazi nyingi zaidi, nimefungwa mara nyingi zaidi, nimepigwa zaidi, na mara nyingi nimekuwa katika hatari ya kufa.
Nao watu wakashangaa sana na kusema: “Mambo anayofanya ni mazuri kweli. Anawawezesha hata viziwi wasikie, nao wabubu wapate kusema.”
Kisha akaingia ndani ya chombo walimokuwa, na upepo ukakoma. Kwa hiyo wanafunzi wakashangaa sana,
Nao waliosikia maneno haya wakasema: “Ni nani basi anayeweza kuokolewa?”
Mutu mumoja akamwuliza: “Bwana, ni watu wachache tu ndio watakaookolewa?” Halafu Yesu akawaambia:
Ni kwepesi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
Yesu akawaangalia na kuwaambia: “Kwa mwanadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si vile, kwa maana mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”