Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Maombolezo 5:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Maana mulima Sayuni umeachwa utupu, mbweha wanazungukazunguka humo.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Maombolezo 5:18
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Akaichoma kwa moto nyumba ya Yawe, nyumba ya kifalme na nyumba zote za Yerusalema; kila nyumba kubwa akaichoma kwa moto.


Halafu tukamwomba Mungu wetu na kuweka ulinzi juu yao, muchana na usiku.


Lakini hao wanaokusudia kupoteza maisha yangu, watatumbukia chini kwenye makao ya wafu.


Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa; Sayuni umekuwa matongo, Yerusalema umekuwa uharibifu.


na juu ya milima katika mbuga. Mali yenu na akiba zenu zote nitazitoa zitekwe kwa kulipia zambi zenu mulizotenda kila pahali katika inchi yenu.


Kwa nini umetabiri kwa jina la Yawe, ukisema kwamba nyumba hii itaharibiwa kama ile ya Shilo na muji huu utakuwa ukiwa, bila wakaaji? Na watu wote wakamuzunguka Yeremia katika nyumba ya Yawe.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninyi mumeona hasara yote niliyouletea Yerusalema na miji yote ya Yuda. Miji hii ni mabomoko mpaka leo wala hakuna mutu anayeishi humo.


Kwa hiyo, kasirani yangu na hasira yangu iliwaka na kumwangika juu ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalema, hata kukakuwa jangwa na mabomoko kama inavyokuwa mpaka leo.


Aliteketeza kwa moto nyumba ya Yawe, nyumba ya kifalme na nyumba zote za Yerusalema; kila nyumba kubwa ilichomwa kwa moto.


Yawe anasema: Nitaifanya Yerusalema kuwa mabomoko matupu, nitaifanya kuwa pango la mbweha; na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa, pahali pasipokaliwa na mutu yeyote.


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


Manabii wenu, enyi Waisraeli ni kama mbweha wanaopitapita katika mabomoko.


Kwa hiyo, ee Mungu, usikilize malalamiko yangu na maombi yangu mimi mutumishi wako. Kwa ajili ya heshima yako, ulionee tena hekalu lako lililoharibika huruma.


Basi! Kwa sababu yenu, Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalema lundo la makokoto, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις