Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Maombolezo 4:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Azabu ya uovu wako, ewe Sayuni imekamilika; Yawe hatawaacha zaidi katika uhamisho. Lakini ninyi Waedomu atawaazibu kwa uovu wenu, atazifichua zambi zenu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Maombolezo 4:22
17 Σταυροειδείς Αναφορές  

Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda, siku ile Yerusalema iliponyanganywa; kumbuka maneno haya waliyosema: “Mubomoe Yerusalema! Muongoe hata na misingi yake!”


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.


Nitafanya nao agano la milele, kwamba sitaacha kuwatendea mema hata kidogo; nitaweka ndani ya mioyo yao utii kwa ajili yangu kusudi wasiniache tena.


Nitawastawisha tena Wayuda na watu wa Israeli; nitawaimarisha kama walivyokuwa hapo zamani.


Nitatakasa zambi zao zote na kuwasamehe uovu wao na uasi walionitendea.


Lakini nimemunyanganya Esau kila kitu, nimeyafunua maficho yake, wala hawezi kujificha tena. Watoto, wandugu na jirani zake wameangamizwa; hakuna hata mumoja aliyebaki.


Siku hizo na wakati huo, uovu utatafutiwa katika inchi ya Israeli, lakini hautapatikana; zambi itatafutiwa katika inchi ya Yuda, lakini haitapatikana; maana mimi nitawasamehe wale ambao nimewaponyesha. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wakaaji wa Edomu, ile inchi ya Uzi, mushangilie na kufurahi kwa sasa. Lakini kikombe hiki cha azabu kitawafikia vilevile. Mutakikunywa na kulewa, hata mutavaa uchi!


Kosa la watu wangu lilikuwa kubwa kuliko zambi za watu wa Sodoma, muji ambao uliteketezwa kwa rafla bila kuwa na muda wa kunyoosha mukono.


Nayo mataifa yatatambua kwamba mimi Yawe, nimewatakasa Waisraeli na kwamba hekalu langu liko kati yao milele.


Anayekuwa mbali sana atakufa kwa ugonjwa mukali. Anayekuwa karibu atauawa kwa upanga. Atakayekuwa amebaki na kuponyoka hayo mawili atakufa kwa njaa. Ndivyo nitakavyotimiza kasirani yangu juu yao.


Kwa sababu ya mateso makali muliyowatendea wandugu zenu wazao wa Yakobo, mutafezeheshwa na kuangamizwa milele.


na kumuchukia Esau. Nimeiharibu inchi ya milima ya Esau ambayo ni urizi wake, nikawaachia imbwa wa pori wa jangwa.


Waedomu, wale wazao wa Esau, wanasema kwamba ingawa miji yao imeharibiwa, watajenga upya mabomoko yake. Lakini, Yawe wa majeshi anasema hivi: Wanaweza kuijenga upya, lakini mimi nitaibomoa tena. Watu watawaita: Taifa ovu ambalo Yawe amelikasirikia milele.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις