61 Umesikia matukano yao, ee Yawe, na mipango yao yote juu yangu.
Kumbuka, ee Yawe, mazarau ya waadui zako; taifa pumbafu linatukana jina lako.
Ee Bwana, yako wapi yale mema yako ya zamani uliyomwahidi Daudi kwa uaminifu wako?
Lakini wewe, ee Yawe, unajua mashauri yao ya kuniua. Usiwasamehe uovu wao, wala kufuta zambi zao. Waanguke chini mbele yako; uwapige wakati wa hasira yako.
Inamupasa kumugeuzia shavu mwenye kumupiga, na kuwa tayari kupokea matusi yake.
Ukumbuke, ee Yawe, mambo yaliyotupata! Utuangalie, uone haya yetu!
Nimeyasikia matusi ya Wamoabu na mazarau ya Waamoni, jinsi walivyowatusi watu wangu na kujivuna kwamba wamenyanganya inchi yao.