Aliteremusha moto kutoka juu, ukanichoma hata ndani ya mifupa yangu. Alinitegea wavu akaninasa, kisha akanirudisha nyuma, akaniacha peke yangu na kuzimia muchana kutwa.
Barabara za Sayuni zinaomboleza, maana hakuna anayepita kwa sikukuu. Milango yake yote ni tupu, makuhani wake wanaugua, wabinti zake wana huzuni, na muji wenyewe uko katika uchungu.