Basi, kwenda umutangazie Israeli maneno haya: Rudi, ewe Israeli usiyekuwa mwaminifu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nami sitakuangalia kwa hasira maana mimi ni mwema. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, sitakukasirikia milele.
Maana mimi niko pamoja nawe, nipate kukuokoa. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote, ambayo niliyokusambaza kati yao; lakini sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakuazibu kadiri unavyostahili wala sitakuachilia uende bila kukuazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.