14 Nimekuwa kitu cha kuchekelewa kwa watu wote, muchana kutwa nimekuwa mutu wa kuzomewa.
Waliotupeleka kuwa watumwa walitaka tuwaimbie; watesaji wetu walitaka tuwafurahishe, wakituambia: “Mutuimbie nyimbo zimoja za Sayuni!”
Umeuzisha watu wako kwa bei ya chini; wala haukupata faida yoyote.
Tunazarauliwa na mataifa jirani, jirani zetu wanatuchekelea na kutusimanga.
Ee Yawe, wewe umenidanganya, nami kweli nimedanganyika; wewe una nguvu kuliko mimi, nawe umeshinda. Nimekuwa mutu wa kuchekelewa kila siku, kila mutu ananizarau.
Ee Moabu, si ulimuchekelea Israeli! Ulimuhesabu kama mwenzake na wanyanganyi hata ukakuwa unatikisa kichwa chako kila mara uliposema juu yake.
Wakiikaa au wakienda, ni mimi ndiye wanayemuzomea.