Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Maombolezo 2:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu. Hawakufichua wazi uovu wako kusudi wapate kukurudishia hali yako ya mbele. Lakini walikuonea maono ya uongo na ya kupotosha.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Maombolezo 2:14
31 Σταυροειδείς Αναφορές  

Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Nao makuhani hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe? Wafundi wa sheria hawakunijua, viongozi wa watu waliniasi; manabii nao walitabiri kwa jina la Bali na kuabudu sanamu zisizokuwa na faida yoyote.


Na kwa upande wako, wewe Pashuri, pamoja na watu wote wanaokaa ndani ya nyumba yako, mutapelekwa katika utumwa. Hakika mutakwenda Babeli na huko ndiko utakapokufia na kuzikwa, pamoja na warafiki zako wote uliowatabiria uongo.


Kama wangalihuzuria katika baraza langu, wangalitangazia watu wangu maneno yangu, wangaliwageuza kutoka katika njia zao mbaya, na kutoka katika matendo yao maovu.


Lakini jambo la “Muzigo wa Yawe”, musilitaje tena. Neno mwanadamu analosema litakuwa muzigo kwake mwenyewe, kwa maana munageuza maneno yangu mimi Mungu Mwenye Uzima, Yawe wa majeshi, Mungu wenu.


Basi, nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania: Sikiliza, Hanania. Yawe hakukutuma, nawe unawafanya watu hawa waamini uongo.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi juu ya Ahabu, mwana wa Kolaya na juu ya Zedekia mwana wa Masea, ambao wanawatabiria uongo kwa jina lake: Nitawatoa katika mikono ya Nebukadneza, mufalme wa Babeli, naye atawaua waziwazi mbele ya macho yenu.


Wako wapi manabii waliokutabiria wakisema: Mufalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala inchi hii?


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Ni kwa sababu ya zambi za manabii wake na makosa ya makuhani wake, ambao walimwanga damu ya watu wa haki katika muji wake.


Kwa sababu mumewavunja watu wa haki moyo kwa kusema uongo, ijapokuwa mimi sikuwavunja moyo, mukawaimarisha waovu wasiache mienendo yao mibaya na kuokoa maisha yao,


Wakubwa wenu ni kama simba anayenguruma anaporarua nyama wake. Wanaua watu, wanawanyanganya watu mali na vitu vyao vya bei kali, na kuongeza hesabu ya wajane.


Manabii wake wanaficha maovu hayo kama mutu anapotia chokaa kwenye ukuta wenye kuharibika. Wanapata maono ya uongo na kutabiri udanganyifu mutupu, wakisema “Bwana wetu Yawe anasema hivi”, wakati mimi mwenyewe sikuwaambia chochote.


Yawe aliniambia: Wewe mwanadamu! Uko tayari kuwahukumu Ohola na Oholiba? Basi, uwatangazie matendo yao ya kuchukiza!


Siku za azabu zimetimia, siku za kulipiza kisasi zimefika; Waisraeli lazima wautambue wakati huo! Ninyi munasema: Nabii ni mupumbafu; anayeongozwa na roho ni mwenda-wazimu. Munasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mukubwa, kwa sababu ya chuki yenu kali juu yake.


Kama mutu angetokea akitangaza maneno matupu ya uongo na kusema “Ninawatabiria divai na pombe kwa wingi”, muhubiri wa namna hiyo angependwa na watu hawa!


Lakini kwa upande wangu, nimejazwa nguvu na roho ya Yawe; nimejaliwa kufuata sheria ya Mungu na kuwa na uwezo niwatangazie wazao wa Yakobo kosa lao, niwaambie Waisraeli zambi yao.


Manabii wake ni watu wasiojali na wadanganyifu. Makuhani wake wamevichafua vitu vitakatifu na kuivunja sheria kwa nguvu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις