Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Maombolezo 1:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Aliyahesabu makosa yangu yote akayakusanya pahali pamoja; aliyafunga katika shingo langu kama nira, nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake. Yawe aliniweka katika mikono ya watu ambao siwezi kuwapinga.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Maombolezo 1:14
21 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


Nitauvunja uwezo wa Waasuria katika inchi yangu; nitawakanyagakanyaga katika milima yangu. Nitawaondolea watu wangu nira yao ya unyanganyi, na muzigo wa mateso yao.


Niliwakasirikia watu wangu, Israeli, nikawafanya watu wangu kuwa wanaharamu. Niliwatia katika mikono yako, nawe haukuwaonea huruma; na wazee uliwabebesha nira nzito sana.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Yeremia akamwambia Zedekia mufalme wa Yuda, mambo hayohayo, akisema: Mukubali kubeba nira mufalme wa Babeli atakayowalazimisha kubeba. Mumutumikie yeye na watu wake, kusudi mupate kuishi.


Lakini kama taifa lolote au utawala wowote hautajiweka chini ya mamlaka ya Nebukadneza mufalme wa Babeli, na kukataa kubeba katika shingo yao zile nira atakazowalazimisha kubeba, basi nitaliazibu taifa hilo kwa vita, njaa na magonjwa makali mpaka nitakapoliangamiza kabisa kwa njia yake. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kwenda umwambie Hanania kwamba: Yawe anasema hivi: Wewe umevunja nira ya muti, lakini mimi nitatengeneza ingine ya chuma.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeweka nira ya chuma ya utumwa kwenye shingo la mataifa yote ya pande hizi, yakuwe katika utumwa, nayo yatamutumikia Nebukadneza, mufalme wa Babeli. Nimemupa Nebukadneza hata nyama wa pori wamutumikie.


Maana Zedekia, mufalme wa Yuda, alikuwa amemufunga Yeremia akisema: Kwa nini unatabiri na kusema: Yawe anasema hivi: Mimi ninautia muji huu katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atauteka.


Zedekia atapelekwa mpaka Babeli, naye atakaa huko mpaka nitakapomushugulikia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kama mukipigana na Wakaldea, hamutawashinda.


mufalme Zedekia alimwita na kumukaribisha kwake. Mufalme akamwuliza kwa siri wakiwa katika nyumba yake: Kuna neno lolote kutoka kwa Yawe? Yeremia akamujibu: Ndiyo, kuko. Kisha akaendelea kusema: Wewe utatiwa katika mikono ya mufalme wa Babeli.


Nitawatoa ndani ya muji na kuwatoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine, nami nitawahukumu.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: tosha kitambulisho chako cha kifalme na taji yako, maana mambo hayatabaki kama yalivyokuwa. Wanaokuwa chini watanyanyuliwa, wanaokuwa juu watashushwa!


Kweli, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakutia katika mikono ya watu unaowachukia, watu unaowaona kuwa kinyaa.


Basi, nitawatoa ninyi katika mikono ya watu wa mashariki; watapiga hema zao kati yenu na kufanya makao yao katika inchi yenu. Nao watakula matunda yenu na kunywa maziwa yenu.


basi, mimi nimeunyoosha mukono juu yenu kwa kuwaazibu; nitawaacha mukamatwe mateka na watu wa mataifa mengine. Nitawaangamiza kabisa, nanyi hamutakuwa taifa tena wala kuwa na inchi. Kwa hiyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efuraimu, kama simba mukali kwa watu wa Yuda. Mimi mwenyewe nitawararua na kuondoka, nitawakamata na hakuna atakayewaokoa.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninapanga kuwaletea ninyi hasara, ambayo hamutaweza kuiponyoka hata kidogo. Utakuwa wakati mubaya kwenu, wala hamutaweza kutembea kwa maringo.


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις