Kwa sababu hii, Yawe akakasirikia sana inchi ya Yuda na Yerusalema, na yale aliyowatendea yalikuwa ya kushangaza, ya kuogopesha na ya kuchekelewa. Haya yote mumeyaona wenyewe kwa macho yenu.
Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.
Kwa hiyo, watu wanaoishi katika miji ya Israeli watatoka na kukusanya silaha zilizoachwa na kuzichoma kwa moto. Watatumia hizo ngao, pinde, mishale, mikuki na magongo, kama kuni za kuwasha moto kwa muda wa miaka saba.
Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.
Ninyi muliona kwa macho yenu mambo ambayo Yawe aliyafanya juu ya Bali-Peori. Yawe, Mungu wenu, aliwaangamiza watu wote kati yenu waliomwabudu huyo mungu Bali-Peori.
Waisraeli waliponililia mimi Yawe, niliweka giza kati yao na Wamisri na kuifanya bahari iwafunike Wamisri. Ninyi wenyewe mulijionea yale niliyowatendea Wamisri. Muliishi katika jangwa muda murefu.