17 Wote wakakula na kushiba. Nao wanafunzi wakaokota vipande vilivyobaki, wakajaza vitunga kumi na viwili.
Mutumishi wake akawatayarishia chakula, wakakula na kushiba, na kingine kikabaki, kama vile Yawe alivyosema.
Yeye anakunywesha wenye kiu; na anashibisha wenye njaa mazuri.
Afazali mali kidogo ya mutu wa haki kuliko utajiri mwingi wa watu waovu.
Mwenye haki yuko na chakula cha kumutoshelea, lakini tumbo la waovu linataabika kwa njaa.
Kisha Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Halafu akaimega, akawapa wanafunzi waigawanyie watu.