Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.
Halafu watu wote wa inchi ya Wagerasi wakashikwa na woga mukubwa, kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke kwao. Basi Yesu akaingia ndani ya chombo, kusudi apate kuondoka kule.