Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 8:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Halafu akawaambia wanafunzi wake: “Imani yenu iko wapi?” Nao wakaogopa na kushangaa, wakiulizana: “Huyu ni mutu gani? Anaamuru hata zoruba na ziwa, navyo vinamutii!”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 8:25
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo katika mukono? Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa? Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake? Uniambie kama unajua!


wakati alipowekea bahari mupaka wake kusudi maji yake yasipate kuvunja amri yake, wakati alipoweka misingi ya dunia.


Mara moja Yesu akanyoosha mukono, akamushika na kumwambia: “Ee wewe mwenye imani ndogo! Kwa sababu gani uliona shaka?”


Yesu akawajibu: “Kwa sababu imani yenu ni ndogo. Kweli ninawaambia kama mukiwa na imani, hata ikiwa tu kama punje ndogo sana ya mbegu ya haradali, mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Toka hapa uende kule,’ nao utatoka pale. Hakuna kitu chochote kitakachokosa kuwezekana kwenu. [


Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana leo na kesho yanatoweka na kutupwa katika moto, hatawavalisha ninyi vizuri zaidi, ninyi wenye imani ndogo?


Yesu aliposikia maneno haya, akashangaa na kuwaambia watu waliomufuata: “Kweli ninawaambia: katika inchi yote ya Israeli, sijaona bado mutu anayekuwa na imani kubwa kama huyu.


Yesu akawajibu: “Sababu gani munaogopa kama hivi? Hakika imani yenu ni ndogo!” Halafu akasimama, akakaripia zoruba na maji na kukakuwa kimya kabisa ndani ya ziwa.


Na ilipotimia magaribi siku ile ile, Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Tuvuke ngambo ingine ya ziwa.”


Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana pale leo na kesho yanatoweka na kutupwa, hatawavalisha vizuri zaidi ninyi wenye imani ndogo?


Basi wanafunzi wake wakamujongelea, wakamwamusha wakisema: “Bwana, Bwana, tunakufa!” Yesu alipoamuka, akakaripia zoruba, nayo ikakoma na maji yakatulia.


Yesu na wanafunzi wake wakaezeka chombo katika inchi ya Wagerasi, kuelekea Galilaya.


Yesu akamwambia: “Sikukuambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις