Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 7:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Katika muji ule kulikuwa mwanamuke mumoja aliyejulikana kuwa mwenye mwenendo mubaya. Mwanamuke yule alipopata habari kama Yesu alikuwa akikula ndani ya nyumba ya yule Mufarisayo, akafika akileta chupa la jiwe linalojaa marasi ya bei kali.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 7:37
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kati ya hawa wawili ni nani aliyefanya sawa na mapenzi ya baba yake?” Wale wakubwa wakajibu: “Ni yule wa kwanza.” Na Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: Walipishaji wa kodi pamoja na makahaba wataingia mbele yenu katika Ufalme wa Mungu.


Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”


Watu wote walioona hayo wakaanza kunungunika wakisema: “Amekwenda kupanga kwa mutenda maovu!”


Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Sikukuja kuwaita wenye haki, lakini wenye zambi kusudi wageuke toka zambi zao.”


Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nanyi munasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki ya walipishaji wa kodi na watenda maovu.’


Siku moja Mufarisayo mumoja akamwalika Yesu kwake kuja kula chakula. Basi Yesu akaenda kwenye nyumba ya yule Mufarisayo, na kuikaa kula chakula.


(Huyu Maria ndiye yule aliyemupakaa Bwana marasi na kupanguza miguu yake na nywele zake, na ni Lazaro kaka yake ndiye alikuwa mugonjwa.)


Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”


Tunajua kwamba Mungu hasikilizi maombi ya wenye zambi, lakini anamusikiliza mutu yule anayemuheshimu na kufanya sawa anavyotaka.


Lakini Mungu ameonyesha wazi upendo wake kwetu ni wapata gani, kwa maana tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.


Neno hili ni la kuaminiwa nalo linastahili kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja katika dunia kwa kuokoa wenye zambi. Na mimi ni wa kwanza mwenye zambi kati yao,


Vilevile ni sherti kujua kwamba Sheria haikuwekwa kwa ajili ya wenye haki, lakini kwa ajili ya watenda mabaya, waasi, watu wasiomuheshimu Mungu, wenye zambi, nao wenye kuchafua vitu vitakatifu na kukufuru, na kwa ajili ya wale wanaowaua wababa zao au wamama zao, na wauaji wowote.


Ni kama vile Maandiko haya Matakatifu yanavyosema: “Ikiwa hata kuokolewa kwa mwenye haki ni kugumu; itakuwa namna gani kwa mwovu na mwenye zambi?”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις