Vilevile hawatii divai mupya ndani ya machupa ya ngozi yenye kuzeeka. Wakifanya vile yale machupa yanapasuka, halafu divai inamwangika, nayo machupa yanapotea bure. Lakini inafaa kutia divai mupya ndani ya machupa mapya ya ngozi, navyo vyote vinalindwa vizuri.”
Vilevile hakuna mutu anayetia divai mupya ndani ya machupa ya ngozi yenye kuzeeka. Kama akifanya vile, ile divai mupya itapasua yale machupa; divai itamwangika na machupa yatapotea bure.
ijapokuwa wandugu wamoja wa uongo waliojiunga nasi kwa kisirisiri walitaka kumutahiri. Watu hao walijiingiza katika kikundi kusudi wapate kupeleleza jinsi tunavyoishi katika uhuru kutokana na kuungana kwetu na Yesu Kristo. Walitaka kututia katika maisha ya kitumwa.
Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.
Basi yule aliyekuwa akiikaa juu ya kiti cha kifalme akasema: “Angalia ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha akaniambia: “Andika maneno haya, kwa maana ni ya kweli na ya uhakika.”