Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 4:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 “Roho wa Bwana yuko pamoja nami, maana amenichagua niwahubirie wamasikini Habari Njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kwamba watakombolewa nao vipofu kwamba wataona. Amenituma kuwapa wanaoteswa uhuru,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 4:18
56 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


kwa sababu umetubu na kunyenyekea mbele yangu, hata umepasua nguo yako na kulia uliposikia maneno yangu juu ya pahali hapa, na juu ya wakaaji wake, na umejinyenyekeza mbele yangu, nami vilevile nimekusikia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


kwamba alichungulia chini kutoka katika pahali pake patakatifu. Yawe aliangalia dunia kutoka mbinguni,


Anawaponyesha waliovunjika moyo; na kuwatunza vidonda vyao.


Wafalme wa dunia wanajitayarisha, watawala wanashauriana pamoja kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.


“Nimemusimika mufalme niliyemuchagua; anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”


Watu wa haki wakimulilia Yawe, yeye anawasikia, na kuwaokoa katika taabu zao zote.


Kiti chako cha kifalme ni imara, kinadumu milele kama cha Mungu. Wewe unatawala watu wako kwa haki.


Ee Bwana, uniwezeshe kusema, midomo yangu itangaze sifa zako.


Macho ya wanaoona hayatapofushwa tena, masikio ya wanaosikia yatabaki wazi.


Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.


Utayafungua macho ya vipofu, utawafungua wafungwa toka katika kifungo, utawaweka huru wale waliofungwa katika giza.


Ni mimi niliyemwamuru Kiro akuje, atimize mapenzi yangu. Nitazifanikisha njia zake zote. Ataujenga upya muji wangu Yerusalema, na kuwapa uhuru watu wangu wanaokuwa katika uhamisho, bila kutaka malipo wala zawadi. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Utawaambia wafungwa: Mutoke humo katika kifungo na wale wanaokuwa katika giza: Mukuje inje kwenye mwangaza! Kila pahali watakapokwenda watapata chakula hata kwenye vilima vitupu watapata malisho.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.


Na agano hilo likavunjwa siku ileile. Wale wachuuzi wa kondoo waliokuwa wananiangalia, wakajua kwamba neno la Yawe lilikuwa limenifikia.


vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.


“Muangalie, mutumishi wangu niliyejichagulia, anayekuwa mupendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitamujaza Roho wangu, naye atatangaza haki yangu kwa mataifa.


Hatavunja tete linalokunja, wala hatazimisha taa inayofifia, mpaka aiwezeshe haki kutawala.


Watu hao wanaokaa katika giza, mwangaza umewatokea! Hao wanaoishi katika inchi yenye giza nzito sana ya lufu, wameona mwangaza mukubwa.”


“Heri wale wanaokuwa wamasikini wa roho, maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!


wakamupa kitabu cha nabii Isaya. Halafu akakifungua na kupata nafasi inayoandikwa:


Kisha Yesu akawaangalia wanafunzi wake na kusema: “Heri kwenu munaokuwa wamasikini, maana Ufalme wa Mungu ni kwenu.


Halafu Yesu akawajibu wale wajumbe: “Mwende kumwelezea Yoane mambo muliyoona na kusikia: vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.


Andrea alimukuta kwanza Simoni, ndugu yake wa tumbo na kumwambia: “Tumemwona Masiya” (maana yake “Kristo”).


Mimi nimekuja katika dunia kama mwangaza, kusudi mutu yeyote anayeniamini asikae katika giza.


Aliyetumwa na Mungu anasema maneno ya Mungu, kwa sababu Mungu anamujaza Roho wake kwa uwingi.


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Wafalme wanajikusanya, wakubwa wanafanya shauri wapate kumwasi Bwana, naye Kristo aliyemuchagua.’


“Ndiyo, ni kweli mufalme Herode, naye mutawala Pontio Pilato walikusanyika katika muji huu pamoja na Waisraeli na watu wa mataifa mengine kwa kufanya shauri baya juu ya mutumishi wako mutakatifu Yesu, uliyemuchagua kuwa Kristo.


Kwa maana yeye ametuokoa toka katika uwezo wa giza, na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mupendwa,


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις