Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Musianze tu kujisemesha kwamba Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 3:8
29 Σταυροειδείς Αναφορές  

Leo hii muwarudishie mashamba yao, mashamba yao ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na nyumba zao, hata na faida ya feza, ngano, divai, na mafuta ambayo mulikuwa munawalipisha.”


Wewe mwanadamu! Wakaaji waliobaki katika miji iliyoharibiwa katika inchi ya Israeli wanasema: Abrahamu alikuwa peke yake, hata hivyo, alipata kurizi inchi hii. Lakini sisi ni wengi; ni wazi tumepewa inchi hii ikuwe yetu!


Kwa sababu hii ninawaambia: Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa kwa watu watakaotoa matunda yanayostahili ufalme ule. [


Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu.


Musijifikiri kwamba munaweza kujidai tu kuwa Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!


“Mwenye nyumba atakapokwisha kusimama na kufunga mulango, ninyi mutabaki inje na kuanza kupiga hodi na kusema: ‘Bwana, utufungulie.’ Naye atawajibu: ‘Sijui munatokea wapi.’


Halafu mutaanza kumwambia: ‘Sisi tulikula na kunywa pamoja nawe, na wewe ulifundisha katika barabara za muji wetu.’


Naye anapokuja, yule aliyewaalika ninyi wawili, ataweza kuja kukuambia: ‘Umwachie mutu huyu kiti.’ Halafu utapatwa na haya kwenda kuikaa kwenye viti vya nyuma.


Yesu akawajibu: “Ninawaambia ninyi: kama watu hawa wakinyamaza, mawe yatalalamika.”


Yesu akamwambia: “Leo nyumba hii imeokolewa, kwa sababu mutu huyu vilevile ni wa uzao wa Abrahamu.


Walimu wa Sheria na Wafarisayo wakaanza kujiuliza: “Ni mutu gani huyu anayemutukana Mungu? Ni nani anayeweza kusamehe zambi, isipokuwa Mungu peke yake?”


Wakamujibu: “Sisi ni wa uzao wa Abrahamu, wala hatujakuwa watumwa wa mutu hata siku moja. Namna gani basi unaweza kutuambia kwamba tutapata uhuru?”


Wakamujibu: “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia: “Kama mungekuwa watoto wa Abrahamu, basi mungefanya matendo yale Abrahamu aliyofanya.


Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.


Kwa hiyo ahadi inafuatana na imani, kusudi ikuwe imetolewa kwa neema ya Mungu. Na zaidi kuwe uhakikisho kwamba ahadi hiyo ni kwa ajili ya wazao wote wa Abrahamu, si kwa wale wanaotii Sheria tu, lakini vilevile kwa wale wanaokuwa na imani kama Abrahamu, babu yetu sisi wote.


wala si wote wanaotoka katika uzao wa Abrahamu, ndio watoto wa kweli wa Abrahamu. Kwa kuwa Mungu alimwahidia Abrahamu: “Ni kwa njia ya Isaka utapata wazao watakaoitwa wako.”


Maisha yenu yatajazwa matendo ya haki ambayo Yesu Kristo anayowajalia, kwa ajili ya utukufu na sifa ya Mungu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις