Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 3:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Basi Yoane akawaambia wote: “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yule atakayekuja nyuma yangu ni mwenye uwezo kunipita; nami sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 3:16
24 Σταυροειδείς Αναφορές  

Musikilize maonyo yangu; nitawamiminia mawazo yangu, nitawajulisha maneno yangu.


Hali itaendelea kuwa hivyo mpaka tujazwe Roho wa Mungu kutoka juu. Hapo jangwa litakuwa shamba lenye udongo muzuri tena, na mashamba yenye udongo muzuri yatakuwa pori.


Bwana atawatakasa wanawake wa Sayuni toka uchafu wao na kusafisha damu iliyomwangika katika Yerusalema, kwa njia ya upepo wa hukumu na wa kuunguza.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Yeye anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”


Yoane akawajibu: “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini kati yenu kuna mutu ninyi musiyemujua,


anayekuja nyuma yangu. Mimi sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”


Mimi sikumujua ni nani, lakini yule aliyenituma kubatiza kwa maji aliniambia: ‘Yule utakayemwona Roho akishuka juu yake na kukaa juu yake, mutu yule ndiye anayebatiza kwa Roho Mutakatifu.’


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: ‘Mito ya maji ya uzima yatatiririka toka ndani ya yule anayeniamini.’ ”


Kwa maana Yoane alibatiza kwa maji, lakini kisha siku chache, ninyi mutabatizwa kwa Roho Mutakatifu.”


Petro alipokuwa hajamaliza kusema maneno hayo, Roho Mutakatifu akashuka juu ya wote waliosikiliza mahubiri yake.


Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.


Vilevile sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, watumwa na watu wanaokuwa huru, tumebatizwa kwa Roho mumoja kusudi tukuwe mwili mumoja na sisi wote tumekunyweshwa Roho mumoja.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις