3 Basi Pilato akamwuliza Yesu: “Wewe ndiwe mufalme wa Wayuda?” Yesu akamujibu: “Ni wewe ndiwe umesema.”
Yesu alipopelekwa mbele ya liwali, yeye akamwuliza: “Wewe ndiwe Mufalme wa Wayuda?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema.”
Kisha wakaanza kumusalimia, wakisema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda!”
Pilato akamwuliza Yesu: “Wewe ni Mufalme wa Wayuda?” Yesu akamujibu: “Umesema.”
Kristo, Mufalme wa Waisraeli, ajishushe sasa juu ya musalaba, kusudi nasi tupate kuona na kumwamini.” Hata wale waliotundikwa pamoja naye walimutukana vilevile.
Wote wakamwuliza: “Basi, wewe ni Mwana wa Mungu?” Yesu akawajibu: “Ninyi munasema kwamba mimi ndiye.”
Na mashitaki haya yalikuwa yameandikwa juu ya musalaba wake: “Huyu ndiye Mufalme wa Wayuda.”
Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”
Kwa hiyo Pilato akawakuta inje, na kuwauliza: “Munamushitaki mutu huyu juu ya nini?”
Wakafika kila wakati mbele yake na kusema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda.” Nao wakamupiga makofi.
Mbele ya Mungu anayevipatia vitu vyote uzima, na mbele ya Kristo Yesu aliyetoa ushuhuda wa kweli mbele ya Pontio Pilato, ninakuagiza maneno haya: