60 Lakini Petro akasema: “Sijui mambo unayoyasema.” Wakati ule alipokuwa angali akisema, jogoo akawika.
Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia kwamba katika usiku huu, mbele jogoo hajawika utakuwa umenikana mara tatu.”
Yesu akamujibu: “Ninakuambia wewe Petro kwamba leo, mbele jogoo hajawika utakuwa umenikana mara tatu kuwa haunijui.”
Kisha muda wa karibu saa moja, mutu mwingine akatia mukazo akisema: “Hakika, mutu huyu alikuwa pamoja naye, kwa sababu yeye ni wa Galilaya.”
Bwana akageuka na kumwangalia Petro. Petro akakumbuka maneno yale Bwana aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika atakuwa amemukana mara tatu.
Lakini Petro akakana tena, na pale pale jogoo akawika.