Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 21:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Lakini mbele mambo hayo yote yatokee, mutakamatwa na kuteswa. Watawapeleka kwenda kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia na kuwatia katika vifungo. Vilevile mutapelekwa mbele ya wafalme na ya wakubwa kwa ajili ya jina langu,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 21:12
31 Σταυροειδείς Αναφορές  

na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatesa na kuwaua.


Na haya yote ni kama mwanzo wa maumivu ya kuzaa tu.


Kutakuwa tetemeko kubwa la inchi. Vilevile kutakuwa njaa na magonjwa makali kwenye nafasi mbalimbali. Zaidi ya ile kutakuwa mambo ya kuogopesha na vitambulisho vya ajabu toka mbinguni.


Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.


Lakini watawafanyia ninyi haya yote kwa ajili yangu, kwa sababu hawamujui yule aliyenituma.


Kesho yake, jemadari alitaka kujua mashitaki kamili ya Wayuda juu ya Paulo. Kwa hiyo akamufungua na kuamuru wakubwa wa makuhani pamoja na Baraza Kubwa wafanye mukutano. Kisha akamuleta Paulo na kumusimamisha mbele yao.


Wajumbe wa baraza wakakubali shauri la Gamalieli. Halafu wakawaita mitume, wakawapiga fimbo na kuamuru wasifundishe tena kwa jina la Yesu. Kisha wakawaacha kwenda.


Lakini Saulo aliendelea kuteketeza kanisa, akiingia nyumba kwa nyumba, na kuwakamata waamini, wanaume na wanawake, na kwenda kuwatupa katika kifungo.


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Kwa ajili ya utukufu wa Bwana, mutii mamlaka yote ya watu: ikiwa ni mufalme anayekuwa na uwezo juu ya vyote,


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις