Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 2:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Kila mwaka wazazi wa Yesu walikwenda Yerusalema kuhuzuria sikukuu ya Pasaka.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 2:41
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Na hivi ndivyo mutakavyokula nyama yule: mutakuwa tayari kwa kusafiri, na kuvaa viatu na kuwa na fimbo zenu katika mikono. Tena mutamukula kwa haraka. Hiyo ni Pasaka ya Yawe.


Vizazi hata vizazi mutakumbuka tukio hilo kwa sikukuu kubwa kwa heshima yangu mimi Yawe. Hilo litakuwa agizo la milele kwenu.”


Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakusanyika mbele ya Bwana wenu, Yawe, Mungu wa Israeli.


Magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza mutafanya kwa heshima yangu mimi Yawe sikukuu ya Pasaka.


Siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza ni Pasaka ya Yawe.


Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, akaenda pamoja nao kule kwa sikukuu ile kama ilivyokuwa desturi.


Sikukuu ya Wayuda ya Pasaka ilikuwa karibu. Basi watu wengi toka katika vijiji wakaenda Yerusalema kusudi wajitakase mbele ya Pasaka.


Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.


Wakati sikukuu ya Pasaka ya Wayuda ilipokaribia, Yesu akaenda Yerusalema.


Na Pasaka, ambayo ni moja ya sikukuu za Wayuda, ilikuwa karibu.


basi huko pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kusudi jina lake likae pale, hapo mutapeleka yote ninayowaamuru: sadaka zenu za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, na sadaka za kutimiza kiapo.


Mutavikula mbele ya Yawe, Mungu wenu, pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua. Mutavikula ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi katika miji yenu.


“Wanaume wote wa taifa lenu watakuja mbele ya Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka, pahali ambapo Yawe, Mungu wenu atachagua: wakati wa sikukuu ya Pasaka, sikukuu ya kuvuna na wakati wa sikukuu ya vibanda. Wasitokee mbele ya Yawe mikono mitupu.


Elekana na jamaa yake yote wakaenda tena Shilo na kumutolea Yawe sadaka ya kila mwaka na kutimiza kiapo.


Kila mwaka Elekana alisafiri kutoka Rama kwenda kuabudu na kumutolea Yawe wa majeshi sadaka kule Shilo. Kule, wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi, walikuwa makuhani wa Yawe.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις