Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 2:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Kisha akabaki mujane, hata akaeneza umri wa miaka makumi nane na mine. Alibaki katika hekalu, akitumikia Mungu usiku na muchana, akifunga kula chakula na kuomba.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 2:37
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Mbona uko mbali sana kwa kunisaidia, mbali na maneno ya kilio changu?


Kweli, uzuri na wema wako vitakuwa pamoja nami siku zote za maisha yangu; nami nitakaa katika nyumba ya Yawe milele.


Jambo moja nimemwomba Yawe, ninatafuta hili tu: nikae ndani ya nyumba ya Yawe siku zote za maisha yangu, niuone uzuri wa Yawe, na kutafuta maongozi yake ndani ya hekalu lake.


Ee Mungu, umwangalie huyo ngao yetu, upendezwe na huyo uliyemuchagua.


Karibu na mazabahu zako, ee Yawe wa majeshi, mufalme wangu na Mungu wangu, hata kichororo ana makao yake, naye mbaruwayi amejenga chicha yake ambamo anaweka vitoto vyake,


Watu wa haki wanastawi kama mingazi; wanakomaa kama mierezi ya Lebanoni!


Kisha akatengeneza birika la shaba na tako lake la shaba. Birika hilo lilitengenezwa kwa kutumia vioo vya shaba vya wanawake waliotumika kwenye mulango wa hema la mukutano.


Watu wamoja wakamwambia Yesu: “Wanafunzi wa Yoane na wale wa Wafarisayo wanafunga mara nyingi na kuomba, lakini wanafunzi wako wanaendelea kula na kunywa.”


Basi wakafunga tena kula chakula na kuomba. Kisha wakaweka mikono juu yao na kuwatuma waende safari.


Wakawachagua wazee katika kila kanisa. Na kisha kuomba na kufunga kula chakula, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana waliyemwamini.


Makabila yetu kumi na mawili wanamwabudu Mungu usiku na muchana, kwa maana wanatumaini kuona utimilifu wa ile ahadi. Na ni kwa sababu ya tumaini lile, Ee mufalme, Wayuda wananishitaki.


Mujane wa kweli asiyekuwa na mutu yeyote wa kumusaidia, anamutumainia Mungu, na kudumu kumutolea mahitaji yake na kumwomba muchana na usiku.


Yule atakayeshinda nitamufanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, naye hatatoka tena mule. Na zaidi ya ile nitaandika juu yake jina la Mungu wangu na jina la muji wa Mungu wangu, ndio Yerusalema mupya, utakaoshuka toka mbinguni kwa Mungu wangu. Nitaandika vilevile juu yake jina langu jipya.


Ndiyo maana wanasimama mbele ya kiti cha kifalme cha Mungu, nao wanamutumikia muchana na usiku katika hekalu lake. Na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme atawalinda katika hema yake.


Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye; hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις