Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 19:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Basi akasema: “Mutu mumoja mwenye heshima alifunga safari kwenda katika inchi ya mbali kusudi asimikwe kuwa mufalme na kisha arudie.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 19:12
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Lakini wakati walimaji walipomwona yule mwana, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue, na shamba hili litakuwa urizi wetu!’


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Kisha Yesu akaanza kusema maneno haya kwa wale wakubwa kwa njia ya mifano: “Mutu mumoja alipanda shamba la mizabibu, akalizungusha na upango, akatengeneza nafasi ya kukamulia matunda ya mizabibu na kujenga munara kwa ajili ya walinzi wa shamba. Kisha akalipangisha kwa walimaji, akaenda safari katika inchi ingine.


Bwana Yesu alipokwisha kusema nao maneno hayo, akanyanyuliwa juu kwenda mbinguni na kuikaa kwa upande wa kuume wa Mungu.


Akaendelea kuwaambia watu mufano huu: “Mutu mumoja alipanda shamba la mizabibu. Kisha kupatana kugawanyana mavuno na walimaji wamoja watakaobaki wakitunza shamba lake, akaenda safari katika inchi ingine na kukaa kule kwa muda murefu.


Alipokuwa akiwabariki akajitenga nao na kunyanyuliwa mbinguni.


Halafu Pilato akamwuliza: “Ni kusema wewe ni mufalme?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema kwamba mimi ni mufalme. Mimi nimezaliwa na kuja katika dunia kusudi nishuhudie ukweli. Wote wanaokuwa upande wa ukweli, wananisikiliza mimi.”


Kwa maana amekwisha kupanga siku atakapohukumu dunia kwa haki, kwa njia ya mutu mumoja, yule aliyemuweka kwa kazi ile. Naye amehakikisha mambo hayo kwa kumufufua mutu yule.”


Kwa maana Kristo anapaswa kutawala mpaka atakapowashinda waadui zake wote na kuwaweka chini ya miguu yake.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


aliyepanda mbinguni, na anayekaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, akitawala wamalaika, nao wenye mamlaka na uwezo wanaokuwa katika mbingu.


Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις