Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 18:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Vilevile Yesu akawaambia mufano huu kwa ajili ya watu waliojiona kuwa wenye haki na kuwazarau wengine.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 18:9
22 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kuna watu ambao wanajiona kuwa safi, kumbe bado hawajatakaswa uchafu wao.


Wanawaambia wale wanaokutana nao hivi: Muikae mbali nami; musinikaribie kwa sababu mimi ni mutakatifu! Watu hao wananikasirikisha sana, hasira yangu ni kama moto usiozimika.


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


Siku ya saba kuhani ataangalia kile kidonda. Kama kidonda hicho hakijaenea na hakuna nywele zenye rangi ya manjano wala hakuna vipele vyovyote pahali pale, basi,


Lakini kwa kutaka kujipatia haki, yeye akamwuliza Yesu: “Mwenzangu ni nani?”


Wafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunungunika, wakisema: “Mutu huyu anawakaribisha watenda mabaya na kula pamoja nao!”


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.


Watu wote walioona hayo wakaanza kunungunika wakisema: “Amekwenda kupanga kwa mutenda maovu!”


Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”


Wayuda wakamujibu: “Sisi tulikuwa na haki ya kusema kwamba wewe ni Musamaria na kwamba uko na pepo.”


Wakamutukana, wakimwambia: “Wewe ndiwe mwanafunzi wa mutu yule! Sisi ni wanafunzi wa Musa.


Wakamujibu: “Wewe, uko mwenye zambi kabisa tangu kuzaliwa kwako! Unataka kutufundisha?” Halafu wakamufukuza inje.


Halafu Bwana akaniambia: ‘Kwenda, kwa maana nitakutuma mbali kwa watu wa mataifa mengine.’ ”


Hawakufahamu namna Mungu anavyowahesabia watu haki na wakatafuta kusimamisha haki yao wenyewe. Wakakataa kufuata njia ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Lakini wewe, kwa sababu gani unamuhukumu ndugu yako? Au wewe kwa sababu gani unamuzarau ndugu yako? Maana sisi wote tutasimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Mungu.


Yule anayekula kila chakula asimuzarau yule asiyekula kila chakula. Vilevile yule asiyekula kila chakula asimuhukumu yule anayekikula, kwa maana Mungu amemupokea.


Zamani nilikuwa muzima pasipo kujua Sheria, lakini wakati amri ilipotokea, zambi ikaanza kutenda kazi,


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις