Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 18:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 18:11
26 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wimbo wa safari za kidini. Mukuje kumusifu Yawe, enyi watumishi wake wote, enyi wote munaotumikia ndani ya nyumba yake usiku.


Mumusifu, enyi munaokaa katika nyumba yake, ndani ya viwanja vya nyumba ya Mungu wetu!


Watu wengi wanajivunia kuwa wema, lakini mwaminifu wa kweli anapatikana wapi?


Kuna watu ambao wanajiona kuwa safi, kumbe bado hawajatakaswa uchafu wao.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Kila siku wananitafuta, wanatamani kujua njia zangu, kama vile wao ni taifa linalotenda haki, taifa lisilosahau agizo la Mungu wao. Wanataka niamue kwa haki, na kutamani kuikaa karibu na Mungu.


Wanawaambia wale wanaokutana nao hivi: Muikae mbali nami; musinikaribie kwa sababu mimi ni mutakatifu! Watu hao wananikasirikisha sana, hasira yangu ni kama moto usiozimika.


Lakini iko wapi ile miungu yenu muliyojifanyia? Basi kama inaweza, isimame iwasaidie, wakati munapokuwa katika shida. Ee ninyi watu wa Yuda, hesabu ya miungu yenu ni sawa na hesabu ya miji yenu!


wewe unasema: Mimi sina kosa; hakika hasira yake imegeuka mbali nami. Lakini mimi nitakuhukumu kwa sababu unasema kwamba haukutenda zambi.


Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.


Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!


kisha Filipo na Bartolomayo, Toma na Matayo aliyekuwa mulipishaji wa kodi; Yakobo mwana wa Alfayo, na Tadeo;


Basi ninawaambia: musipokuwa wenye haki kuliko walimu wa Sheria na Wafarisayo hamutapokelewa katika Ufalme wa mbinguni.


“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Na munaposimama kwa kuomba, mukiwa na neno na mutu mwingine, mumusamehe, kusudi Baba yenu anayekuwa mbinguni, awasamehe vilevile makosa yenu. [


Wananyanganya mali ya wajane na kuomba maombi marefu kusudi waonekane mbele ya watu. Kwa sababu hii watahukumiwa vikali sana!”


Kisha akajitenga nao na kuenda kwenye hatua ya mutu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba akisema:


Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”


nilikuwa na bidii sana hata nilitesa kanisa. Kuelekea mambo ya kuhesabiwa kwa njia ya kushika Sheria, mimi sikupatikana na kosa lo lote.


Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις