Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.
Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.
Kwa maana ikiwa kukataliwa kwao na Mungu kumeleta upatanisho kati yake na dunia, basi si hakika kwamba kukubaliwa kwao na Mungu kutaleta uzima kwa wale waliokufa.
Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.
Hapana hata kidogo! Sherti Mungu ajulikane kuwa mwenye ukweli, na kila mutu kuwa mwongo, kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ee Mungu, sherti ujulikane kuwa mwenye haki katika masemi yako. Nawe ushinde wakati unaposhitakiwa.”