25 “Kwa wakati ule, mwana wake wa kwanza alikuwa kwenye mashamba. Alipokuwa akirudia na kukaribia nyumba, akasikia sauti ya watu wakiimba na kucheza.
Mumusifu kwa ngoma na michezo, mumusifu kwa filimbi na kinanda!
Wanafanana na watoto wanaoikaa kwenye nafasi ya makutano wanaowaita wenzao, wakisema: ‘Tuliwapigia ngoma, lakini hamukucheza! Tuliimba wimbo wa kilio, lakini hamukulia!’
Nitakurudisha katika hali mupya, ewe binti Israeli! Utazitwaa tena ngoma zako, nawe utajitokeza tena kwa kucheza na wenye shangwe.
wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,
Mulisifu jina lake mukicheza, mumwimbie kwa ngoma na zeze.
Wimbo wa safari za kidini. Yawe alipoturudisha tena Sayuni, tulikuwa kama watu wanaoota ndoto!
Daudi alikuwa amejifungia kizibao cha kuhani katika kiuno chake. Alicheza kwa nguvu zake zote mbele ya Yawe.
Basi nabii Miriamu, dada ya Haruni, akatwaa ngoma katika mukono, na wanawake wengine wote wakamufuata wakiwa na ngoma zao ndogo wakicheza.
Usikie, ee Yawe, unihurumie; ee Yawe, unisaidie!”
Kwa sababu mwana wangu huyu alikuwa amekufa, na amefufuka, alikuwa amepotea na sasa ameonekana.’ Nao wakaanza kufurahi pamoja.
Akamwita mumoja kati ya watumishi, na kumwuliza juu ya mambo yanayopitika kule.