Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.
Lakini ninyi mukafurahi na kusherehekea. Mulichinja ngombe na kondoo, mukakula nyama na kunywa divai. Ninyi mulisema: Acha tukule na kunywa maana kesho tutakufa.
Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!
Yule mudogo akamwambia baba yake: ‘Baba, unipe ile sehemu ya urizi inayopaswa kuwa yangu.’ Basi baba akagawanya mali yake kati ya wana wake wote wawili.
Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu: “Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyekuwa na mulinzi wa mali yake. Yule mulinzi akachongewa kwa bwana wake kwamba anaponda mali yake.
Watalipwa mateso kwa sababu ya mateso waliyoleta. Wanafurahia kutimiza waziwazi tamaa zao mbaya za kimwili muchana kati. Kufika kwao katika karamu zenu kunaleta haya na chukizo kubwa wanapofurahia mambo yao ya udanganyifu.