Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 15:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Vilevile ninawaambia, ndivyo wamalaika wa Mungu wanavyofurahi kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 15:10
23 Σταυροειδείς Αναφορές  

Basi, ninafurahia kufa kwa mutu mwovu? Hapana! Mimi ninapendelea aachane na njia zake mbaya apate kuishi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Sifurahii kifo cha mutu yeyote. Hivyo mugeuke kusudi mupate kuishi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


“Kila mutu anayenikubali mbele ya watu, nami nitamukubali vilevile mbele ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [


Ni hivi vilevile Baba yenu anayekuwa mbinguni hataki hata mumoja wa hawa wadogo kupotea.


“Nami ninawaambia: kila mutu anayenikubali mbele ya watu, Mwana wa Mutu atamukubali vilevile mbele ya wamalaika wa Mungu.


Lakini mutu yeyote anayenikana mbele ya watu, yule atakanwa mbele ya wamalaika wa Mungu.


Hakika si vile: lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao.”


Yesu akaendelea kuwaambia mufano mwingine: “Mutu mumoja alikuwa na wana wawili.


Vilevile ninawaambia, ndivyo kutakuwa furaha kubwa zaidi mbinguni kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake, kuliko wenye haki makumi tisa na tisa wasiokuwa na lazima ya kugeuka toka zambi zao.


Anapokipata atawaita warafiki na jirani zake na kuwaambia: ‘Mufurahi pamoja nami kwa sababu nimepata kikoroti kile cha feza nilichokipoteza!’


Ni kwa sababu hii ninakuambia kwamba upendo ambao mwanamuke huyu alioonyesha unahakikisha kwamba Mungu amemusamehe zambi zake zinazokuwa nyingi. Lakini yule anayesamehewa kwa machache haonyeshi upendo zaidi.”


Wandugu waamini waliposikia maneno hayo, wakatulia na kumusifu Mungu, wakisema: “Kumbe Mungu amewajalia hata watu wa mataifa mengine vilevile kusudi waweze kugeuka toka zambi na kupata uzima kamili.”


Lakini usiku malaika wa Bwana akafungua milango ya kifungo, akawaondosha mitume mule na kuwaambia:


Basi, huzuni inayosababishwa na Mungu inamuwezesha mutu kugeuka toka katika zambi. Na kugeuka kule, kunamuletea kuokoka. Kule kuokoka hakuleti majuto. Lakini huzuni inayosababishwa na mwanadamu inaleta kifo.


Labda hii ndiyo sababu Onesimo aliachana nawe kwa muda, kusudi upate tena kuwa naye siku zote.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις