14 Hivi utabarikiwa, kwa maana watu hawa hawana cha kukulipa. Utalipwa hayo yote wakati wenye haki watakapofufuka.”
Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.
Ninatumaini toka kwa Mungu sawa vile watu hawa wanavyotumaini, kwamba watu wema na wabaya wote watafufuliwa.
na kutoka ndani ya makaburi yao. Waliotenda mema watafufuka na kupata uzima, lakini waliotenda mabaya watafufuka na kuhukumiwa.
Hivi tendo lile halitatoka inje, naye Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.
Lakini wakati unapofanya karamu, uwaalike wamasikini, vilema, viwete na vipofu.