Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 12:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 “Ninawaambia ninyi warafiki zangu: musiwaogope wale wanaoua mwili tu lakini hawawezi kufanya kitu kingine zaidi.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 12:4
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama.


Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.


Kinywa chake kinajaa maneno matamu. Yeye wote anapendeza. Basi, hivi ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa, ndivyo rafiki yangu anavyokuwa, enyi wabinti wa Yerusalema.


Sikiliza ewe Israeli, mutumishi wangu, wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua, wewe wa uzao wa Abrahamu, rafiki yangu;


Sasa basi, wewe Yeremia ujiweke tayari. Simama! Uende kuwaambia mambo yote ninayokuamuru. Usiwaogope, kusudi mimi nisikufanye kuwa mwoga mbele yao.


Wewe usiwaogope watu hao. Niko pamoja nawe kwa kukulinda. –Ni ujumbe wa Yawe.


walikuwa wanawaogopa Wakaldea tangu wakati Isimaeli mwana wa Netania, alipomwua Gedalia mwana wa Ahikamu ambaye mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika kuwa mutawala wa inchi.


Lakini, ewe mwanadamu usiwaogope hao wala maneno yao; maana uko katikati ya michongoma na miiba, nawe unaikaa pamoja na nge; usiogope maneno yao wala usitishwe na nyuso zao, maana hao ni watu waasi.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Hakuna anayekuwa na upendo mukubwa kuliko mutu anayetoa maisha yake kwa ajili ya warafiki zake.


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Musiogope waadui zenu hata kidogo. Hii itakuwa kitambulisho kwao kwa kuhakikisha kwamba wanapotea, lakini kwenu ni kwamba munaokolewa. Na hii inatoka kwa Mungu.


Na maandiko haya yakatimia: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa hiyo akahesabiwa kuwa mwenye haki.” Na Mungu akamwita rafiki yake.


Hata mukiteswa kwa ajili ya haki, ninyi ni wenye heri. Musiwaogope watu, wala musihangaike.


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις