Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 12:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 “Wakati watakapowapeleka kwa kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia, au mbele ya watawala na ya wakubwa, musijihangaishe juu ya maneno mutakayojibu au yale mutakayosema,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 12:11
14 Σταυροειδείς Αναφορές  

Basi, kwenda! Mimi nitaongoza kinywa chako na kukufundisha cha kusema.”


Kwa sababu hiyo, nitawatumia manabii na watu wenye hekima na walimu. Mutawaua wamoja wao, mutatundika wengine juu ya misalaba, mutawapiga wengine fimbo ndani ya nyumba zenu za kuabudia na kuwafukuza muji kwa muji.


“Ni kwa sababu hii ninawaambia ninyi: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwa ajili ya chakula au kwa ajili ya kinywaji, wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu kwamba mutavaa nini. Uzima ni wa lazima kuliko vyakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


Nani kati yenu, kwa ajili ya kujisumbua kwake, anaweza kujiongezea hata siku moja kupita muda wa maisha yake?


“Kwa sababu gani munajisumbua kwa ajili ya nguo? Muangalie maua jinsi yanavyoota. Hayatumiki wala kujisukia nguo.


“Basi musijisumbue kwa ajili ya chakula, kwa ajili ya kinywaji au kwa ajili ya nguo.


Basi musijisumbue kwa ajili ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Kila siku ina masumbuko yake inayoitoshelea.


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ni kwa sababu hii ninawaambia: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwamba mutakula nini; wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu, kwamba mutavaa nini.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις