Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 11:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Wakati watu wengi walipokuwa wakikusanyika pembeni ya Yesu, yeye akaanza kusema: “Watu wa kizazi hiki kibaya wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataonyeshwa kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha Yona.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 11:29
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Naye Ezekieli atakuwa kitambulisho kwenu: mutafanya kila kitu kama vile alivyotenda. Wakati mambo hayo yatakapotukia, mutatambua kwamba mimi ni Bwana wenu Yawe.


Neno la Yawe lilimufikia Yona mwana wa Amitai kusema hivi:


Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?


Kwa hiyo mutu yeyote anayesikia haya juu yangu na juu ya mafundisho yangu kati ya watu wa kizazi hiki kisichokuwa na uaminifu mbele ya Mungu na chenye zambi, Mwana wa Mutu atasikia haya juu yake vilevile. Itakuwa vile, atakapokuja pamoja na wamalaika watakatifu, akitukuzwa na Baba yake.”


Na wengine walitaka kumupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake umetoka kwa Mungu.


Basi watu wa kizazi hiki watabeba lazima ya damu ya manabii wote iliyomwangwa tangu kuumbwa kwa dunia,


Wakati ule ule makundi mengi ya maelfu ya watu walikusanyika hata wakakanyaganakanyagana. Yesu akaanza kwanza kusema na wanafunzi wake, akiwaambia: “Mufanye angalisho na chachu ya Wafarisayo, maana yake unafiki wao.


Na Yesu akajibu: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Umulete mutoto wako hapa.”


Basi Wayuda wakamwuliza: “Utaonyesha kitambulisho gani kwa kutuhakikishia kwamba uko na haki ya kufanya hivi?”


Wakamwuliza: “Basi utatuonyesha kitambulisho gani kusudi tupate kukiona na kukuamini? Utafanya jambo gani?


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Wayuda wanaomba kuonyeshwa vitambulisho nao Wagriki wanatafuta hekima.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις