Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.
Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.
Kwa maana hamukupewa roho anayewafanya muishi katika utumwa na kuwatia tena woga, lakini mulipewa Roho anayewafanya mukubaliwe kuwa watoto wa Mungu. Na kwa uwezo wa Roho huyo, tunaweza kumwita Mungu “Baba.”
Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.
Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.