Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Luka 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 kwa maana atahesabiwa kuwa mutu mukubwa mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kinywaji kikali, na atajazwa na Roho Mutakatifu tangu kuzaliwa kwake.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Luka 1:15
22 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Lakini baba yake akakataa, akisema: “Ninajua, mwana wangu, ninajua. Wana wa Manase vilevile watakuwa taifa na wakubwa. Hata hivyo, ndugu yake mudogo atakuwa mukubwa kuliko yeye na wazao wake watakuwa mataifa mengi.”


Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye heshima kama vile wakubwa wengine wa dunia.


Utajiri na heshima vinatoka kwako, vyote unavitawala. Uwezo na nguvu viko katika mukono wako, nawe unawatukuza wale unaowapenda, na kuwaimarisha wote.


Wanasema: “Alimutegemea Yawe, basi, Mungu amuponyeshe! Kama Mungu anapendezwa naye, basi, amwokoe!”


Mbele ya kukutengeneza katika tumbo la mama yako, mimi nilikujua; mbele haujatoka katika tumbo, nilikuweka kwa kazi yangu; mimi nilikuchagua kuwa nabii kwa mataifa.


Lakini wao wakajibu: Sisi hatukunywi divai, maana Yonadabu mwana wa Rekabu, babu yetu, alituamuru hivi: Musikunywe divai; musikunywe ninyi wenyewe wala wana wenu milele.


Munapoingia ndani ya hema la mukutano, wewe na wana wako musikunywe divai wala kileo chochote, kama sivyo mutakufa. Hili litakuwa sharti ambalo vizazi vyenu vyote wanapaswa kulifuata siku zote.


Yawe wa majeshi atawalinda watu wake, nao watawaangamiza waadui zao. Watapiga kelele katika vita kama walevi, wataimwanga damu ya waadui zao. Itatiririka kama damu ya nyama wanaotolewa kwa sadaka iliyomiminwa juu ya mazabahu kutoka ndani ya bakuli.


Utakuwa na furaha na shangwe kwa ajili yake, na watu wengi watafurahia kuzaliwa kwake,


Ninawaambia: kati ya watu wanaoishi katika dunia, hakuna anayekuwa mukubwa kuliko Yoane. Lakini yeyote anayehesabiwa kuwa mudogo katika Ufalme wa Mungu anahesabiwa kuwa mukubwa kuliko yeye.”


Ni hivi vilevile, Yoane Mubatizaji alikuja, yeye anafunga kula chakula na kunywa divai, nanyi munasema: ‘Yuko na pepo.’


Yoane alikuwa kama taa inayowaka na kuangaza, na ninyi mulipendezwa kufurahishwa na mwangaza wake kwa muda.


Wote wakapewa Roho Mutakatifu na kuanza kusema kwa luga mbalimbali kwa kadiri Roho alivyowawezesha kusema.


Lakini, Mungu aliyenichagua mbele sijazaliwa na kuniita kwa neema yake, alipendezwa


Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.


Yawe akamwambia Yoshua: “Leo hii, nitaanza kukutukuza mbele ya watu wote wa Israeli kusudi wajue kwamba, kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo vilevile nitakavyokuwa pamoja nawe.


Katika siku hiyo Yawe akamutukuza Yoshua mbele ya Waisraeli wote, nao wakamuheshimu Yoshua maisha yake yote kama walivyomuheshimu Musa katika maisha yake.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις