Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Kutoka 10:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Musa akamujibu: “Kila mutu, vijana na wazee, tutaondoka na watoto wetu wanaume na wanawake, kondoo na mbuzi wetu na ngombe. Kwa maana tunapaswa kumufanyia Yawe sikukuu.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Kutoka 10:9
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri, wakamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke, wanifanyie sikukuu katika jangwa.’ ”


“Wao watakusikiliza, nawe pamoja na wazee wa Waisraeli mutamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: ‘Yawe, Mungu wa Waebrania, ametutokea. Sasa, uturuhusu tuende safari ya mwendo wa siku tatu katika jangwa, tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka.’


Na ninyi wababa musiwakasirikishe watoto wenu. Lakini muwalee na kuwaonya, mukiwatolea mashauri yanayotoka kwa Bwana.


Ukumbuke Muumba wako siku za ujana wako wakati hazijafika siku mbaya wala haijakaribia miaka utakaposema: “Sina furaha katika vitu hivyo.”


Umuheshimu Yawe kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote.


Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”


Siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mutafanya mukutano mutakatifu. Hamutafanya kazi siku hiyo. Mutafanya sikukuu kwa ajili ya Yawe kwa siku saba.


Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, na katika siku ya saba mutafanya sikukuu kwa heshima ya Yawe.


Musa na Haruni wakamwambia: “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tunakusihi utuache tujiendee katika jangwa mwendo wa siku tatu tutoe sadaka kwa Yawe, Mungu wetu. Kama sivyo, yeye atatuua kwa ugonjwa mukali au kwa upanga.”


Vilevile, Yosefu alisindikizwa na jamaa yake yote, wandugu zake na jamaa yote ya baba yake Yakobo. Katika eneo la Goseni kulibaki watoto wao tu pamoja na kondoo, mbuzi na ngombe wao.


Mufalme wa Misri akawaambia: “Basi, Yawe akuwe pamoja nanyi kama nitawaruhusu mujiendee na watoto wenu. Ni wazi kwamba muko na nia mbaya ndani ya moyo wenu.


Ngombe wetu tunapaswa vilevile kuwapeleka wala hakuna hata nyama mumoja atakayebaki nyuma. Kwa sababu kutoka katika mifugo yetu wenyewe, tutamutumikia Yawe, Mungu wetu, wala sisi hatujui ni nyama gani tutakayemutolea Yawe sadaka mpaka tutakapofika kule.”


Mutwae makundi yenu ya kondoo na ngombe, muondoke. Muniombee na mimi baraka.”


Waisraeli waliondoka katika muji wa Ramesesi, wakasafiri kwa miguu kuelekea Sukoti. Walikuwa wanaume yapata elfu mia sita, bila kuhesabu wanawake na watoto.


Kulikuwa vilevile kundi la watu wengine waliokwenda pamoja nao na mifugo mingi, kondoo na ngombe.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις