Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe akamwambia Isaya: Uende pamoja na mwana wako anayeitwa Watakaobaki-Watarudi, kukutana na mufalme Ahazi. Utamukuta katika barabara pahali wafuaji wa nguo wanapofanyia kazi, mwisho wa mufereji unaoleta maji kutoka kwenye birika la juu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 7:3
14 Σταυροειδείς Αναφορές  

Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, Ahazi mwana wa Yotamu, mufalme wa Yuda, akaanza kutawala.


Kisha mufalme wa Asuria alimutuma majemadari wakubwa watatu pamoja na kundi kubwa la waaskari kutoka Lakisi kwenda kwa mufalme Hezekia kule Yerusalema. Walisafiri na kufika Yerusalema. Nao walipofika waliingia na kusimama karibu na mufereji wa kisima kinachokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea kiwanja cha mufuaji wa nguo.


Matendo mengine ya Hezekia, ushujaa wake na maelezo juu ya jinsi alivyojenga kisima na kuchimba mufereji wa kuleta maji katika muji, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.


Sehemu inayofuata mpaka kwenye makaburi ya Daudi, kisima na majengo ya waaskari ikajengwa upya na Nehemia mwana wa Aibuki, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Beti-Suri.


Basi, kwenda ukutane naye kesho asubui, wakati anapokwenda kwenye muto Nili. Umungojee kando ya muto. Utwae katika mukono wako ile fimbo iliyogeuka kuwa nyoka.


Wazao wa Yakobo wachache watakaobaki watamurudilia Mungu Mukubwa.


Mulizikagua nyumba za Yerusalema, mukazibomoa kwa kupata mawe ya kukaza kuta za muji.


Katikati ya kuta hizo mulijijengea birika la kulinda maji yanapotiririka kutoka birika la zamani. Lakini hamukumutafuta Mungu aliyepanga mambo haya yote; hamukumujali yeye aliyepanga hayo yote tangu zamani.


Kisha mufalme wa Asuria alimutuma jemadari kutoka Lakisi na kundi kubwa kumwendea mufalme Hezekia. Jemadari yule alisimama karibu na mufereji wa birika linalokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea shamba la wafuaji wa nguo.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.


Yawe anasema hivi: Kwenda kwa jamaa ya kifalme ya Yuda, na utoe ujumbe huu kule:


Isaya alisema kwa sauti juu ya Waisraeli: “Ijapokuwa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaookolewa.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις