Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 66:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Katika kila sikukuu ya mwandamo wa mwezi, na katika kila siku ya Sabato, wanadamu wote watakuja kuniabudu. –Ni Yawe anayesema hivyo.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 66:23
25 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mume wake akamwuliza: “Kwa nini unataka kumwona leo? Leo si sikukuu ya mwandamo wa mwezi wala Sabato.” Akamujibu: “Si neno.”


Ulimwengu wote utakumbuka na kumurudilia Yawe; jamaa zote za mataifa zitamwabudu.


Ee Mungu, unastahili sifa huko Sayuni. Watu wanapaswa kukutimizia viapo vyao,


maana wewe unajibu maombi yetu. Wanadamu wote watakuja kwako wewe peke.


Mataifa yote uliyoumba, yatakuja kukuabudu, ee Bwana; yatatangaza ukubwa wa jina lako.


Yawe atajijulisha kwa Wamisri na hapo ndipo Wamisri watakapomwitikia na kumwabudu kwa kumutolea matoleo na sadaka za kuteketezwa. Vilevile watafanyia Yawe viapo ambavyo watavitimiza.


Wakati huo, kutakuwa barabara kubwa kutoka inchi ya Misri mpaka katika inchi ya Asuria. Waasuria watawatembelea Wamisri, na Wamisri watawatembelea Waasuria; nao wote watamwabudu Mungu pamoja.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Siku hiyo, baragumu kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea katika inchi ya Asuria au waliotawanywa katika inchi ya Misri watarudi na kumwabudu Yawe juu ya mulima mutakatifu kule Yerusalema.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Maana, katika mulima wangu mutakatifu, mulima murefu wa Israeli, ninyi wote watu wa Israeli mutanitumikia kule. –Ni ujumbe wa Yawe.– Huko mimi nitawapokea na kungojea muniletee sadaka na matoleo yenu bora na matoleo iliyotakaswa.


Itakuwa ni mapaswa ya mufalme kuhakikisha kuwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za vyakula na sadaka za kinywaji zinazotolewa wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi, Sabato, na sikukuu zozote zilizowekwa kwa Waisraeli, zinapatikana. Mufalme yeye mwenyewe atatayarisha sadaka za kusamehewa zambi, sadaka za vyakula, sadaka za kuteketezwa kwa moto, na sadaka za amani kwa kuwafanyia watu wote wa Israeli upatanisho.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mulango wa kiwanja cha ndani unaoelekea upande wa mashariki utafungwa siku zote sita za kazi. Siku za Sabato na siku za mwandamo wa mwezi utafunguliwa.


Wakati wa sikukuu ya mwandamo wa mwezi atatoa mwana-ngombe dume, wana-kondoo sita, na kondoo dume mumoja; wote wasiokuwa na kilema.


Watu wa Yuda watapigana kwa kuulinda Yerusalema; utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka inchi ya Yuda utakusanywa: watakusanya zahabu, feza na nguo kwa wingi sana.


Kisha, kila mutu aliyebaki kati ya mataifa yote yaliyokuja kuushambulia Yerusalema, atakuwa akikuja Yerusalema mwaka kwa mwaka, kwa kumwabudu Yawe wa majeshi anayekuwa mufalme, na kushiriki kwa sikukuu ya Vibanda.


Ikiwa Wamisri watakataa kushiriki kwa sikukuu ya Vibanda, basi, Yawe atawapiga kwa ugonjwa uleule atakaowapiga nao mataifa yote yanayokataa kushiriki kwa sikukuu hiyo.


Hiyo itakuwa ndiyo azabu itakayolipata taifa la Misri pamoja na mataifa yote yasiyoshiriki kwa sikukuu ya Vibanda.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Lakini kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wale wanaoabudu kwa kweli watakapomwabudu Baba katika roho na ukweli; kwa maana Baba anataka watu wanaoabudu kwa namna ile.


Ewe Bwana, hakuna asiyekuogopa, wala hakuna asiyekutukuza, kwa maana wewe peke yako ndiwe mutakatifu. Mataifa yote yatakuja kukuabudu, kwa maana matendo yako ya haki yameonyeshwa wazi.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις