Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 61:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Wazao wao watajulikana kati ya mataifa; watajulikana kati ya watu wengine. Kila mutu atakayewaona atakubali kwamba wao ni watu waliobarikiwa na Yawe.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 61:9
15 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”


Lakini Labani akamwambia: “Basi uniruhusu nami niseme. Nimetambua kwa kuaguza kwamba Yawe amenibariki kwa sababu yako.


Yawe awajalie muongezeke; awajalie muongezeke ninyi na wazao wenu!


Musiogope maana mimi nipo pamoja nanyi. Nitawarudisha wazao wenu toka mashariki, nitawakusanya ninyi kutoka magaribi.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.


Kazi zao hazitakuwa bure, wala hawatazaa watoto watakaopatwa na musiba; maana watakuwa waliobarikiwa na Yawe, wamebarikiwa wao pamoja na wazao wao.


Kama vile mbingu mupya na dunia mupya nitakazoumba zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu, ndivyo wazao wako na jina lako litakavyodumu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Maana Yawe anasema hivi: Mushangilie kwa furaha kwa ajili ya Yakobo, mupige vigelegele kwa ajili ya taifa kubwa, mutangaze, musifu na kusema: Yawe ameokoa watu wake, ameleta ukombozi kwa wale waliobaki kati ya Waisraeli!


Enyi watu wa Yuda na watu wa Israeli! Wakati uliopita ninyi mulionekana kuwa watu waliolaaniwa kati ya watu wa mataifa. Lakini sasa mimi nitawaokoa, nanyi mutakuwa watu waliobarikiwa. Basi, musiogope tena, lakini mujipe moyo!


Halafu mataifa yote yatawaita ninyi watu waliobarikiwa, maana inchi yenu itakuwa inchi ya furaha. –Ni Yawe, Mungu Mukubwa anayesema hivyo.


Mungu akamwambia Balamu: Usiende pamoja na watu hawa, wala usiwalaani watu hao maana wamebarikiwa.


Hivi Mungu alimutuma mutumishi wake kwa ajili yenu kwanza, kusudi awabariki ninyi, akimugeuza kila mumoja wenu toka katika njia zake mbaya.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις