Mungu akamwambia yule mutu aliyevaa nguo ya kitani: Kwenda katikati ya magurudumu yanayokuwa chini ya makerubi, ujaze mikono yako na makaa ya moto unaokuwa katikati yao na kuyasambaza juu ya muji. Nikamwona akienda.
Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.
Sisi tuko na mazabahu yetu, nao makuhani Wayuda wanaotumika katika Pahali Patakatifu hawana ruhusa ya kula sehemu ya vitu vinavyotolewa sadaka juu ya mazabahu ile.