Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 56:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Heri mutu anayefuata maneno hayo, anayeshika kabisa siku za Sabato kwa heshima na kuepuka kutenda uovu wowote.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 56:2
31 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nikawakaripia viongozi wa watu wa Yuda, nikisema: “Uovu gani huu munaofanya, kuichafua siku ya Sabato?


Heri wale wanaofuata sheria ya Mungu, wanaotenda siku zote mambo ya haki.


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


Ninajizuiza kufuata njia mbaya, kusudi nipate kushika neno lako.


Wimbo wa safari za kidini. Heri wote wanaomwabudu Yawe, wanaoishi kufuatana na amri zake.


Basi, uache kusema mabaya, na kuepuka kusema uongo.


Achana na uovu, utende mazuri, nawe utaishi katika inchi siku zote;


Lakini siku ya saba ni Sabato ya Yawe, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mutumwa wako, wala mujakazi wako, wala nyama wako wa kufugwa, wala mugeni anayekuwa katika nyumba yako.


Usisahau kuiweka takatifu siku ya Sabato.


Mwenye hekima ni mwangalifu na anaepuka uovu, lakini mupumbafu hajizuizi wala hana uangalifu.


Njia ya watu wa usawa ni kujiepusha na uovu; anayechunga njia yake anachunga maisha yake.


Kwa wema na uaminifu mutu anaondoa uovu. Kwa kumwogopa Yawe anaepuka ubaya.


Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke, uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.


Usigeukie kuume wala kushoto; epusha muguu wako mbali na uovu.


Inakupasa ushike neno la kwanza na la pili vilevile; maana anayemutii Mungu atayaepuka yote.


Maana Yawe anasema hivi: Towashi anayeshika siku zangu za Sabato, anayefanya mambo yanayonipendeza, na kuchunga agano langu,


Wageni watakaoshikamana nami Yawe, kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu, na kuwa watumishi wangu, wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua, watu watakaofuata agano langu,


Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato, ukiacha shuguli zako siku yangu hiyo takatifu, ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha, ukiheshimu siku hiyo takatifu ya Yawe, ukiacha shuguli zako au kupiga domo,


Niliwapa vilevile Sabato zangu zikuwe kitambulisho kati yangu na wao, wapate kujua kwamba mimi ni Yawe ninayewatakasa.


Mufanye Sabato zangu kuwa takatifu, kusudi zikuwe kitambulisho cha agano langu nanyi. Hizo zitawakumbusha kwamba mimi Yawe ni Mungu wenu.


Mutashika Sabato zangu na kuheshimu Pahali pangu Patakatifu. Mimi ni Yawe.


Lakini Yesu akajibu: “Heri zaidi wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii!”


Heri mutumishi yule, ikiwa saa bwana wake anaporudia, anamukuta akifanya kazi ile.


Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.


Upendo wenu ukuwe pasipo udanganyifu. Muchukie chochote kinachokuwa kibaya, mushikamane na kinachokuwa chema.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις