Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 55:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 55:3
45 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nitafanya nao agano la milele, kwamba sitaacha kuwatendea mema hata kidogo; nitaweka ndani ya mioyo yao utii kwa ajili yangu kusudi wasiniache tena.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


Mwana wangu, sikia kwa uangalifu maneno yangu, utegee sikio masemi yangu.


Kondoo wangu wanasikia sauti yangu, ninawajua, nao wananifuata.


Na juu ya ufufuko wa Yesu, kusudi asipate kuoza, Mungu alisema: ‘Nitakupa baraka takatifu zinazokuwa za hakika, nilizomwahidia Daudi.’


“Nitasimamisha agano langu nawe, wazao wako na vizazi vyao vyote milele; nitakuwa Mungu wako na Mungu wa wazao wako milele.


Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Mashairi ya Asafu. Musikie mafundisho yangu, enyi watu wangu, mutegee sikio maneno ya kinywa changu.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Munapaswa kushika masharti yangu na maagizo yangu: yule anayeyashika ataishi. Mimi ni Yawe.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Anayekuwa mutu wa Mungu anasikia maneno ya Mungu. Hamusikii, kwa sababu ninyi si watu wa Mungu.”


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Watauliza njia ya kwenda Sayuni, na nyuso zao zikielekea huko, wakisema: Mukuje! Nao watajiunga na Yawe katika agano la milele ambalo halitasahauliwa hata kidogo.


Basi, ndivyo inavyokuwa vilevile: sitawatupa wazao wa Yakobo na Daudi, mutumishi wangu; nitamuchagua mumoja kati ya wazao wake atawale wazao wa Abrahamu, Isaka na Yakobo. Kwa maana nitawarudishia tena hali yao na kuwahurumia.


Nao hawatakuwa tena watumwa wa wageni, lakini watanitumikia mimi Yawe, Mungu wao pamoja na mufalme wa ukoo wa Daudi ambaye nitakayewasimikia.


Nimekusudia kwa moyo wote kufuata masharti yako milele.


Nami nitamufanya kuwa muzaliwa wangu wa kwanza, mukubwa kuliko wafalme wote wa dunia.


Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.


“Lakini heri kwenu, kwa sababu macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia!


Haya ndiyo mambo Musa aliyoandika juu ya kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria: “Mutu anayetimiza maagizo ya Sheria, ataishi kwa njia yake.”


Siku ya mwisho ya sikukuu ile iliyokuwa siku kubwa, Yesu akasimama na kusema hivi kwa sauti: “Mutu akiwa na kiu, akuje kwangu akunywe.


“Ee Yawe, Mungu, usimugeuzie masiya wako mugongo. Kumbuka wema wako kwa mutumishi wako Daudi.”


Unijalie kuishi nipate kukusifu; na maamuzi yako yanisaidie.


Munisikilize, enyi watu wangu, munitegee sikio, enyi taifa langu. Sheria na haki zitatoka kwangu mimi; nazo zitakuwa mwangaza wa mataifa.


Milima inaweza kutoweka, vilima vinaweza kuondolewa, lakini rehema zangu kwako sitaziacha, agano langu la amani litaimarishwa. Ni Yawe anayekuhurumia anayesema hivyo.


Yeremia akamujibu: Hautatolewa kwao. Wewe sasa utii kile Yawe anachosema, kama ninavyokuambia, na mambo yote yatakuendekea vema, na maisha yako yataokolewa.


Lakini mimi nitalikumbuka agano langu nililoagana nawe katika siku za ujana wako. Nitafanya nawe agano la milele.


Nami Yawe, nitakuwa Mungu wao, naye mutumishi wangu Daudi atakuwa mukubwa wao. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Nitafanya nao agano la amani, nalo litakuwa agano la milele. Nitawabariki na kuwafanya wakuwe wengi, nami nitaweka hekalu langu kati yao milele.


Yawe anawaambia Waisraeli hivi: Munitafute mimi nanyi mutaishi!


Mutafute Yawe, nanyi mutaishi! Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto; moto utawateketeza wakaaji wa Beteli na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha.


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Kwa hiyo, ninakuomba nyumba yangu mimi mutumishi wako ipate kudumu milele mbele yako. Wewe umesema. Kwa baraka zako nyumba yangu itabarikiwa milele.”


Nitamwonyesha wema wangu kwa milele, na agano langu kwake litadumu siku zote.


Ufuate amri zangu nawe utaishi; ulinde mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.


Nitafanya nao agano la amani. Nitaondoa nyama wakali katika inchi, kusudi kondoo wangu wakae katika mbuga kwa usalama na kulala katika pori.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις