Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 52:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Katika hali ya sasa ninapata faida gani kuwaona watu wangu wamepelekwa katika utumwa? –Ni ujumbe wa Yawe. Hao wanaowatawala wanajitapa. Nalo jina langu linaendelea kuzarauliwa kila siku. –Ni ujumbe wa Yawe.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 52:5
27 Σταυροειδείς Αναφορές  

Hata hivyo, kwa sababu kwa tendo lako umemuzarau kabisa Yawe, mutoto wako atakufa.”


Umetufanya kama kondoo wanaopelekwa kuchinjwa; umetutawanya kati ya mataifa.


Muchana kutwa nimefezeheka, na uso wangu umejaa haya tele


Ee Mungu, mpaka wakati gani adui atakuchekelea? Watakufuru jina lako milele?


Kumbuka, ee Yawe, mazarau ya waadui zako; taifa pumbafu linatukana jina lako.


Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,


Una haki gani kuwa huku? Una ndugu yeyote hapa, hata ukajichongea kaburi ndani ya jiwe juu ya mulima?


Lakini, ninakujua wewe Saniharibu; ninajua wakati unaikaa, wakati unatoka, na wakati unaingia; ninajua vilevile wakati kasirani yako inawaka juu yangu.


aliwaambia: “Mumwambie bwana wenu kwamba Yawe anasema hivi: Usiogope kwa sababu ya maneno uliyoyasikia, ambayo watumishi wa mufalme wa Asuria wameyasema kwa kunitusi.


Niliwakasirikia watu wangu, Israeli, nikawafanya watu wangu kuwa wanaharamu. Niliwatia katika mikono yako, nawe haukuwaonea huruma; na wazee uliwabebesha nira nzito sana.


Watoto wako wamezimia, wamelala pembeni ya kila barabara, wako kama paa aliyenaswa ndani ya mutego. Wamepatwa na kasirani ya Yawe, wamepatwa na azabu ya Mungu wako.


Nami nitakitia katika mikono ya wanaokutesa, waliokuambia ulalie tumbo wapite juu yako, nawe ukaufanya mugongo wako kama vile udongo wa njia, kama vile barabara ya kupitia.


Yawe anasema hivi: Ninyi muliuzishwa bure bila malipo yoyote, na mutakombolewa bila kulipa feza.


Israeli ni kama kondoo wanaowindwa na kufukuzwa na simba. Kwanza waliangamizwa na mufalme wa Asuria, na sasa Nebukadneza mufalme wa Babeli, amevunjavunja mifupa yake.


Sikiliza ninavyolalamika; hakuna wa kunifariji. Waadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu: wanafurahi kwamba umeniletea hasara. Uifanye ile siku uliyoahidi ifike, uwafanye nao wateseke kama mimi.


Ameivunja kwa hasira nguvu yote ya Israeli. Hakunyoosha mukono kwa kuwasaidia walipokutana na adui; amewawakia watu wa Yakobo kama moto, akateketeza kila kitu.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Siku hiyo, kutasikilika kilio kutoka Mulango wa Samaki, maombolezo kutoka Mutaa wa Pili, na mulio mukubwa kutoka katika milima. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kwa maana kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu yenu, jina la Mungu linatukaniwa katikati ya watu wa mataifa mengine.”


Walipokuwa kwa Mika, wakaitambua sauti ya yule kijana Mulawi. Wakamugeukia na kumwuliza: “Nani amekuleta huku? Una shuguli gani hapa?”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις