Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Isaya 52:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe anasema hivi: Ninyi muliuzishwa bure bila malipo yoyote, na mutakombolewa bila kulipa feza.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Isaya 52:3
13 Σταυροειδείς Αναφορές  

Umetufanya kama kondoo wanaopelekwa kuchinjwa; umetutawanya kati ya mataifa.


Umeuzisha watu wako kwa bei ya chini; wala haukupata faida yoyote.


Muji Sayuni utakombolewa kwa njia ya kufuata sheria ya Mungu, nao wakaaji wake waliogeuka toka zambi zao kwa njia ya haki.


Ni mimi niliyemwamuru Kiro akuje, atimize mapenzi yangu. Nitazifanikisha njia zake zote. Ataujenga upya muji wangu Yerusalema, na kuwapa uhuru watu wangu wanaokuwa katika uhamisho, bila kutaka malipo wala zawadi. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.


Ninyi mutaitwa: Watu Watakatifu, Watu waliokombolewa na Yawe. Nawe Yerusalema utaitwa: Muji Mungu anaoupenda, Muji ambao Mungu hakuuacha.


Niliamua kwamba siku ya kulipiza kisasi imefika; wakati wa kuwakomboa watu wangu umefika.


Yawe anasema: Nitazifanya mali zenu na akiba zenu zitekwe tena, wala hamutapewa malipo yoyote ya vitu hivyo kwa sababu ya zambi zenu zote mulizozitenda kila pahali katika inchi.


Umejijengea nafasi yako yenye kuinuka kwa mwanzo wa kila barabara na kujijengea pahali pa kutambikia katika kila kiwanja. Tena wewe haukukuwa kama kahaba maana ulikataa kulipwa.


Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Lakini ikiwa mutu huyu na jamaa yake hakukombolewa kwa njia hizo, basi apewe uhuru wake katika mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano.


Kwa maana munajua namna gani mulivyokombolewa toka katika tabia za ovyo ovyo mulizoambukizwa na babu zenu. Hamukukombolewa kwa njia ya vitu vinavyoharibika kama vile feza au zahabu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις