Isaya 51:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Mukumbuke Abrahamu babu yenu, na Sara aliyewazaa ninyi. Abrahamu alikuwa hana mutoto wakati nilipomwita, lakini nilimubariki na kumufanya kuwa na wengi.
Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!
Kwa hiyo, Yawe aliyemukomboa Abrahamu, anasema hivi juu ya wazao wa Yakobo: Wazao wa Yakobo hawatapata haya tena, hawatainamisha vichwa vyao tena kwa ajili ya haya.
Musikilize, enyi watu wa Yakobo, enyi munaojulikana kwa jina la Israeli, ninyi munaokuwa wa uzao wa Yuda. Ninyi munaapa kwa jina la Yawe, na kudai kwamba munamwabudu Mungu wa Israeli; lakini hayo si ukweli wala sawa.
Anayekuwa jamaa ndogo kati yenu atakuwa kabila, anayekuwa mudogo kuliko wote atakuwa taifa kubwa. Mimi ndiye Yawe; wakati utakapofika nitayatimiza haraka.
Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.
Wewe mwanadamu! Wakaaji waliobaki katika miji iliyoharibiwa katika inchi ya Israeli wanasema: Abrahamu alikuwa peke yake, hata hivyo, alipata kurizi inchi hii. Lakini sisi ni wengi; ni wazi tumepewa inchi hii ikuwe yetu!
utasema maneno haya mbele ya Yawe, Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Musuria aliyetangatanga huko na huko, kisha akashuka kwenda Misri akaishi huko kama mugeni. Yeye na jamaa yake walikuwa watu wachache tu walipokuwa huko, lakini wakakuwa taifa kubwa lenye nguvu na watu wengi.